2 Chronicles 12:1-6

Shishaki Ashambulia Yerusalemu

(1 Wafalme 14:25-28)

1 aBaada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mwenyezi Mungu. 2 bKwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu. 3 cAkiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi
Yaani watu kutoka sehemu ya Naili ya juu.
yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 eAkateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.

5 fNdipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’ ”

6 gViongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mwenyezi Mungu ni mwenye haki.”

Copyright information for SwhKC